![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEht14U5mqVf8xTsPwi6u6m6Nh56rdsGC-RCIzCx9p9hyphenhyphen3NOhaVGnBde-UoUvnGMO8-g1tFGYJwriAan4Ooho8mamrFMNxLx0Jgfo0lTP3C8GdTR_3y-mAsJ_Bbq79sQTWFJhI0TAlzzFkuQ/s400/Maji-machafu-600x350.jpg)
mengine nchini vimelalamikiwa kwa kutoweka mazingira salama kwa watu
wanaoishi maeneo jirani.
Baadhi ya malalamiko
hayo ni pamoja na viwanda vilivyopo katika eneo la Boko CCM, Basihaya Jijini
Dar es Salaam, wawekezaji wa China wanaotafuta madini Wilayani Mkuranga mkoani
Pwani na Kiwanda cha Saruji Songwe ambacho kiko jirani na Uwanja wa Ndege Songwe
ambacho kinalalamikiwa kwa tatizo la vumbi kuathiri usalama wa abiria wanaofika
katika uwanja huo pamoja na wakazi wanaozungukwa na eneo hilo.
Viwanda hivyo huchafua
mazingira kwa kutiririsha maji machafu na kutumia baruti kupasua miamba
katika maeneo hayo. Wakazi wa maeneo ya Boko CCM wameeleza kuwa wamepata shida
hiyo kwa muda mrefu na kwamba hakuna mikakati madhubuti ya kudhibiti hali hiyo
ambayo ni pamoja na kulipwa fidia wananchi ambao wameathiriwa na uwepo wa
viwanda hivyo.
Hata hivyo, kilio cha
wananchi wanaozungukwa na viwanda hivyo kwa Serikali ni kusikilizwa kwa
madhara wanayoyapata na kuacha tabia ya kuvifungia kwa muda mfupi viwanda hivyo
baada ya kubainika kuwa vimekiuka kanuni za uhifadhi wa mazingira
Baraza la Uhifadhi wa
Mazingira (NEMC) limekuwa likivifungia viwanda hivyo kwa muda mfupi,
jambo ambalo limekemewa na wakazi hao wakitaka adhabu kali zaidi itolewe kwa
viwanda husika.
Zipo baadhi ya kampuni
na viwanda nchini ambavyo pamoja na kupewa onyo na mamlaka zinazohusika, bado
zimeendelea kuchafua mazingira kwa kutiririsha maji yanayoathiri binadamu na
mifugo, jambo ambalo linahatarisha afya za wananchi katika maeneo wanayoishi.
Mmoja wa wakazi wa
jiji la Mbeya aliyejitambulisha kwa jina la Gladness Bakari, amesema
taka ambazo zinaweza kusababisha matatizo ya afya ni pamoja na za viwandani,
taka ngumu kama vifuko ya plastiki, vinyesi na hata vumbi la migodini na kadhalika,
huku akisisitiza kuwa athari hizo zinaweza kuwa za kimwili, mikrobiyolojia,
biyolojia au kemikali ambazo ni vikolezo vya magonjwa.
Akizungumza Mwanasheria wa NEMC,
Heche Suguta, amekiri kuwa baraza hilo limekuwa likipokea malalamiko mengi
kutoka kwa wakazi ambao wanavizunguka viwanda hivyo pamoja wakilalamikia vumbi
na kelele kuwaathiri kiafya.
Pamoja na hayo amekiri
kwamba Baraza lilijulishwa kuwa uchafuzi unaofanywa na baadhi ya viwanda Jijini
Dar es Salaam (hakutaja jina) umesababisha watoto kupata mafua yasiyoisha,
kukohoa, kuumwa vichwa na Kifua Kikuu (TB), walilalamikia wakati mwingine
kushindwa hata kulala kutokana na hali hiyo.
Kiwanda cha MMI Steel kinacholalamikiwa kwa uchafuzi wa mazingira
Viwanda hivyo vimekuwa
zikiamriwa kulipa mara moja faini isiyopungua milioni 40 kwa kuvunja kifungu
namba 191 cha sheria ya mazingira ya mwaka 2004. Kiwanda cha Saruji Songwe
ambacho kiko jirani na uwanja wa ndege Songwe, Mbeya ni moja ya viwanda
vinavyolalamikiwa kwa tatizo la vumbi kuathiri wakazi wanaozungukwa na kiwanda
hicho.
Shirika la Afya
Duniani (WHO), mwaka 1992, lilitoa kauli kwamba licha ya sekta ya viwanda kukua
na kuwa miongoni mwa sekta mama katika kukuza uchumi na kupunguza tatizo la
ajira, ujenzi holela wa viwanda jirani na makazi ya watu ni hatari kwa afya za
wananchi.
Mkazi wa Jiji la Dar
es Salaam, Shafii Haruna, anayeishi karibu na moja wapo ya kiwanda kinachofanya
uzalishaji wa bidhaa za mafuta ya kupaka na sabuni ameelezea namna
anavyonufaika na kiwanda hicho na hatari inayomnyemelea kuwa ni pamoja viwanda
hivyo kutiririsha maji machafu katika mifereji inayochezwa na watoto
wadogo ambao hawana uelewa wa madhara ya maji hayo.
Kwa mujibu wa mkazi
huyo, wananchi jijini humo wanatakiwa kuhakikisha wanathamini matumizi ya
nishati mbadala ili kupunguza matumizi ya kuni na madhara yanayotokana na
viwanda.
Serikali kupitia Ofisi
ya Makamu wa Rais – Mazingira, imevitaka viwanda nchini kujenga utaratibu
wa kutathmini afya za wananchi ambao ndiyo chimbuko la maendeleo ya taifa
lolote duniani.
“Wananchi wabadilishe
matumizi ya nishati kwa kutumia kuni na mkaa kwa kuzingatia teknolojia muhimu
zilizopo sasa kwamaana watatumia kiasi kidogo cha kuni, viwanda vizingatie
uzalishaji bora wa bidhaa na kupunguza uzalishaji joto na kuwa na mifumo mizuri
ya maji taka” kilieleza chanzo chetu kutoka katika Ofisi hiyo.
Taarifa kutoka kwenye
Ofisi hiyo zinabainisha kuwa, wakati hayo yakitokea bado Serikali ipo kwenye
mkakati wa kutengeneza mazingira kwa ajili ya kuwavutia wadau wa maendeleo
kwenda kuwekeza kwenye mikoa ya pembezoni wakati hali ilivyo katika miji na
majiji bado ikiwa hairidhishi.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgarHHnrNHIvYE22sONiBWQWeikNbZoCAfhqOOus0juWK-swI8PVi8WgjSA8239JavGyhMd4MrcLe8ydOIcXbBJpJgcr-NK98zHYn_NOufYvhQuxWWUFoC37NTKdshU9QOigEt3tlFIupkF/s400/uchafu-mmi-steel.jpg)
Barabara inayolalamikiwa kumwagiwa mabaki ya malighafi zinazozalishwa katika kiwanda cha kutengeneza Nondo na Mabati cha MMI STEEL cha Jijini Dar es Salaam
Kumbukumbu zinaonyesha
kuwa chini ya sheria ya kimataifa kuhusu Haki za Binadamu, serikali zina wajibu
mwingi katika kulinda haki za kuishi za raia yao.
Azimio la haki za binadamu kote ulimwenguni (Universal
Declaration of Human Rights), makubaliano ya Kimataifa Juu Ya Haki Za Kiuchumi
na Kijamii Na Kiutamaduni (International Covenant on Economic and Social and Cultural
Rights-ICESCR) na Mkataba Juu Ya
Haki Za Watoto (Convention on the Rights of the Child -CRC) zote zinaweka haki ya kupata hali nzuri sana
ya afya iwezekanayo chini ya mkataba huu wa ICESCR, inajumuisha wajibu wa
kuboresha afya ya mazingira, kuwalinda wananchi dhidi ya hatari za kiafya
katika mazingira, kuhakikisha mazingira ya kazi yenye afya na kulinda haki ya
kupata chakula na maji safi.
Dunia ya leo inakabiliwa na ongezeko la joto duniani, uharibifu
wa mazingira na matatizo mengine kama vile machafuko, vita na mauaji ya mtu
mmoja mmoja na ya kimbari, ugaidi, uvamizi na ukaliaji wa kimabavu wa nchi moja
dhidi ya nyingine, Utengenezaji wa silaha za maangamizi (WMD), nyukilia, za
kibaiolojia na nyinginezo. Tatizo kuu linalosababisha haya ni mtu kaacha au
kapunguza uhusiano wake wa kiutu na mazingira yake.-FIKRA PEVU
No comments:
Post a Comment