Mamlaka hiyo pia inapokea maoni ya wananchi kupitia:
- Kuchangia maoni kwenye mkutano utakaofanyika Januari 5, 2016 katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam kuanzia saa 3 na nusu asubuhi
- Ofisi ya Mkurugenzi Mkuu wa SUMATRA, S.L.P 3093, Dar es Salaam.
- Barua pepe: info@sumatra.go.tz
- Maoni ya maandisi yatapokelewa kwenye ofisi ya Mkuregenzi Mkuu iliyopo Jengo la Mawasiliano House (Makutano ya barabara ya Ali Hassani Mwinyi na Nkumo), kuanzia saa 4 asubuhi hadi saa 9 alasiri.
Mwisho wa kupokelewa maoni ni Januari 13 mwaka huu.
Mamlaka hiyo imepokea maombi ya nauli kutoka kampuni ya UDA-RT inayolenga kutoa huduma ya mpito ya usafirishaji jijini Dar es Salaam katika kutekeleza awamu ya kwanza ya mradi wa DART. Maombi yaliyowasilishwa na kampuni hiyo ni safari kwenye njia za pembeni (feeder route) shilingi 700, safari kwenye njia kuu (trunk route) shilingi 1,200 na njia zote mbili ni 1,400 ambapo wanafunzi watalipa nusu nauli anayotoa mtu mzima.
No comments:
Post a Comment