Baadhi ya wananchi na wanaCCM wakiwa wamemsimamisha mgombea mwenza wa CCM nafasi ya urais, Mama Samia Suluhu Hassan Kata ya Igagala, Uvinza Mkoani Kigoma wakimtaka awasalimie kabla ya kuendelea na safari. Mgombea mwenza huyo wa CCM ameingia mkoani Kigoma kwa ziara ya kampeni kuinadi ilani ya CCM.
Baadhi ya Wananchi wakiwa wamesimama pemezoni mwa barabara kumlaki mgombea mwenza wa urais CCM alipokuwa akiwasili Mkoani Kigoma kufanya mikutano yake ya kampeni.
Mgombea mwenza akizungumza na wananchi waliomsimamisha njiani kuwasilisha kero zao.
Mgombea mwenza CCM, Mama Suluhu akiwa ameshikilia kadi na bendera za vyama vya upinzani alizokabidhiwa na vijana waliohama vyama vyao na kujiunga na CCM, alipokuwa akiwasili Mkoani Kigoma mwisho wa reli
No comments:
Post a Comment