.

.
TZ WAKA BLOG TUNAKUTAKIA HERI YA MWAKA MPYA 2016, MWAKA HUU UWE WA BARAKA NA MAFANIKIO KWAKO | KUTANGAZA NA BLOG HII WASILIANA NASI KUPITIA 0716 979 939 AU BARUA PEPE tzwakablog@gmail.com

07 September, 2015

Lowassa: "Sina muda wa kujibu matusi na kejeli zinazotolewa na CCM"

MGOMBEA urais wa Tanzania anayewakilisha Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), Edward Lowassa amesema hana muda wa kujibu matusi na kejeli zinazotolewa na viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) dhidi yake.

Badala yake amesema anatumia muda uliobaki wa kampeni kutafuta kura kwa wananchi kwa kunadi ilani ya chama chake. 

Lowassa aliyeteuliwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ameeleza hayo katika mkutano wa kampeni kwenye viwanja vya Mbezi Mwisho, jimbo la Kibamba, jijini Dar es Salaam.

Kauli hiyo ameitoa kama mrejesho wa kampeni ya kimkakati inayofanywa na makada wa CCM walioamua kumshambulia wakimtuhumu kuwa hafai urais, ni kapi, fisadi na mgonjwa.

SOMA HABARI KAMILI

No comments: