.

.
TZ WAKA BLOG TUNAKUTAKIA HERI YA MWAKA MPYA 2016, MWAKA HUU UWE WA BARAKA NA MAFANIKIO KWAKO | KUTANGAZA NA BLOG HII WASILIANA NASI KUPITIA 0716 979 939 AU BARUA PEPE tzwakablog@gmail.com

24 October, 2015

DAWA ZA KULEVYA AINA YA HEROINE NA COCAINE ZATEKETEZWA CHINI YA UANGALIZI MKALI JIJINI DAR


 Sehemu ya Kinu cha Kiwanda Cha Saruji Cha Wazo Hill Jijini  Dar es Salaam  ambako dawa za kulevya zimeteketezwa jana chini ya uangalizi mkali . Akizungumza  na waandishi wa habari mara baada ya kuzichoma moto katika kinu hicho Jaji  wa Mahakama Kuu Edison Mkasimongwa alizitaja aina ya dawa hizo kuwa  ni Heroine mifuko 179 na Cocaine mifuko 81 zenye thamani ya Shilingi Bilioni tano ambapo  zilikuwa na Gram 175,000 ambazo zilikamatwa miaka kadhaa Mbezi Jogoo jijini Dar.
Jaji wa Mahakama Kuu Edison Mkasimongwa(kulia) akihakiki sehemu ya kinu cha kuchomea madawa hayo ya kulevya uku akisindikizwa na Mkurugenzi wa Mashtaka  Biswalo Mganga(kushoto) katika Kiwanda Cha Saruji Cha Wazo Hill Jijini  Dar es Salaam
Hii ndio sehemu ya mfuniko wa kinu kilichotumika kuchomea dawa za kulevya
Majaji kutoka mahakama kuu pamoja na polisi wakifuatilia kwa umakini uteketezaji wa dawa za kulevya

No comments: