KUHUSU VYAMA NA WAGOMBEA KUZINGATIA MAADILI YA UCHAGUZI WA RAIS, WABUNGE NA MADIWANI YA MWAKA 2015
Kama mnavyofahamu Kampeni za Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani zimeanza tangu tarehe 22 Agosti, 2015 na zinaendelea hadi tarehe 24 Oktoba, 2015.
Ni jambo linaloeleweka kwamba mchakato wa Kampeni na wa Upigaji Kura unatawaliwa au kuongozwa na Sheria, Katiba na Maadili ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani ya mwaka 2015.
Katika kipindi hiki tangu Kampeni zianze, nafurahi kusema kwa niaba ya Tume kuwa kwa ujumla, Kampeni zimeenda vizuri. Karibu mikutano yote imefanyika katika hali ya utulivu na amani. Hatujapata taarifa ya mkutano wa Kampeni ambao umevurugwa kwa fujo zozote. Kwa hilo napongeza Vyama vyote vya Siasa.
Hata hivyo, kutokana na mikutano hiyo nchini ya Kampeni, ngazi ya Urais, Ubunge na Udiwani yamejitokeza mambo ambayo ni kinyume kabisa na Mwongozo wa Maadili ya Uchaguzi wa Rais Wabunge na Madiwani wa mwaka 2015 uliotiwa saini na Vyama vyote vya Siasa tarehe 27 Julai, 2015.
No comments:
Post a Comment